Wednesday, October 23, 2013


SIFA ZA UFALME WA MILENIA

Sehemu ya II.

Karibu tena ndugu msomaji wa blogu hii ya AMINI TU! (Only believe!) Katika somo lililopita tulijifunza juu ya Ufalme wa milenia na sifa zake. Habari za ‘Ufalme wa milenia’ zipo katika kitabu kile cha Ufunuo wa Yohana ukianzia Sura ya 19 hadi ya 20. (Tazama pia Waefeso 1:10)


Kwa leo tunaendelea na sehemu ya pili baada ya kuona kuwa sisi kama Kanisa la Kristo, tu mawakala wa ufalme wa Mungu.  Tuliona kuwa moja ya sifa za Ufalme wa Millenia ni Yesu mwenyewe kuwa mtawala kwa kipindi cha miaka 1000! (Ufunuo 20:4). Katika kipindi hiki sifa kubwa sana ni kwamba kutakuwa na amani kuu!
·         Amani Kuu- ni sifa ya ufalme wa MILENIA.

Katika Mika 4:1-2 na Isaya 2:4; na 51:11 Biblia inaweka wazi kuwa kipindi cha milenia kitakuwa kipindi cha amani tele tele! Tena inabaibisha wazi kwamba huzuni zote “zitakimbia”.

 ·         Ufahamu wa Ki-mungu- ni sifa nyingine ya kipindi hiki.

Kutakuwa na kunjua Mungu kwa namna ambayo kutaijaza dunia yote kipindi chote ambacho Mfalme Mkuu Yesu Kristo atakapo tawala pale Yerusalem –Israel. ( Isaya 11:1-9) (Dunia itajawa na kumjua Bwana kama maji yanavyoifunika bahari!)

·         Watu wote watayafanya mapenzi ya Mungu maana watamjua.

Hii nayo ni sifa ya kipindi hiki. Bwana atatawala kutokea Yerusalem na atatawala “kwa fimbo ya chuma” ikimaanisha atatawala kwa haki na hukumu. (Isaya9: 6-7; Mika 4:3).

Mwisho wa Ufalme wa Milenia ni baada ya miaka 1000 ya utawala wa Kristo hapa duniani. Baada ya miaka hiyo ufalme wa milemnia utachukua sura mpya ya “Ufalme wa Mungu”. Huu utadhihirika kwa matukio makuu matatu:

a)    Shetani atafunguliwa baada ya ile miaka 1000 ya kifungo chake (maana kipindi cha Millenia hatafurukuta) (Ufunio 20:1-3). Wakati huo atajipanga kufanya vita (a final show down) dhidi ya Bwana Yesu Kristo na watakatifu (wateule) lakini atashindwa kabisa katika vita hiyo kuu sana. Yapo mataifa ambayo yatashikamana na Ibilisi kupigana na Kristokatika kipindi hichi cha mwisho baada ya milenia lakini watashindwa – Ufunuo 20:7-10 inabainisha haya.


b)   Shetani (Ibilisi) atakomeshwa kabisa na ufalme wake utaondolewa na kukoma kabisa!

 
c)    Waovu wote watahukumiwa na kutiwa hatiani kwa yale yote yaliyotendwa katika mwili. Hii ni hukumu ya mwisho (tz.Ufunuo 20:11-15). Haya yote yatatokea wakati wa mwisho baada ya kipindi cha milenia kumalizika. Watu wote ambao hawataonekana katika “Kitabu Cha Uzima Cha Mwana-kondoo” watatupwa katika ziwa la moto, nah ii inaitwa “mauti ya Pili” maana watatengwa na Mungu aliye hai milele na milele!

Ni muhumu basi, ndugu msomaji wangu mpendwa, kuzingatia sana habari za wokovu huu tuliopewa. Maandika yanasema  sis je tutapata je kupona tusiojali wokovu huu? Kumbuka kuwa pazia la wokovu lilianza pale Eden na kudhihirika pale Golgotha! Baadae litakunjwa au  kufungwa baadaye – yaani Mungu ataufunga ukurasi wa maisha ya dunia hii. Je umesha fanya maauzi ya wapi utakuwa umeangukia? Je ni katika ziwa la moto au ni katika Paradiso ya Kristo? Katika hayo mawili unapaswa kuyafanyia maamuzi. Uamuzi wa kumchagua Yesu na kuingizwa katika kitabu cha Uzima cha Mwanakondoo ni wa maana zaidi kuliko kuishi bila uhakika wa maisha ya sasa na yale ya baadae.

Mungu akubarikie kwa kusoma na kuchukua hatua. Kwa maswali zaidi, niandikie: nangela04@yahoo.co.uk au fuatilia katika blogu hii.

No comments:

Post a Comment