SIFA
ZA UFALME WA MILENIA
Sehemu
ya II.
Karibu tena ndugu
msomaji wa blogu hii ya AMINI TU! (Only believe!) Katika somo lililopita
tulijifunza juu ya Ufalme wa milenia na sifa zake. Habari za ‘Ufalme wa
milenia’ zipo katika kitabu kile cha Ufunuo
wa Yohana ukianzia Sura ya 19 hadi ya 20. (Tazama pia Waefeso 1:10)
Kwa leo tunaendelea
na sehemu ya pili baada ya kuona kuwa sisi kama Kanisa la Kristo, tu mawakala
wa ufalme wa Mungu. Tuliona kuwa moja ya
sifa za Ufalme wa Millenia ni Yesu mwenyewe kuwa mtawala kwa kipindi cha miaka
1000! (Ufunuo 20:4). Katika kipindi
hiki sifa kubwa sana ni kwamba kutakuwa
na amani kuu!
·
Amani
Kuu- ni sifa ya ufalme wa MILENIA.
Katika Mika 4:1-2 na Isaya 2:4; na 51:11 Biblia
inaweka wazi kuwa kipindi cha milenia kitakuwa kipindi cha amani tele tele!
Tena inabaibisha wazi kwamba huzuni zote “zitakimbia”.
Kutakuwa na kunjua
Mungu kwa namna ambayo kutaijaza dunia yote kipindi chote ambacho Mfalme Mkuu
Yesu Kristo atakapo tawala pale Yerusalem –Israel. ( Isaya 11:1-9) (Dunia itajawa na kumjua Bwana kama maji
yanavyoifunika bahari!)
· Watu wote watayafanya mapenzi ya Mungu maana watamjua.
Hii nayo ni sifa ya
kipindi hiki. Bwana atatawala kutokea Yerusalem na atatawala “kwa fimbo ya
chuma” ikimaanisha atatawala kwa haki na hukumu. (Isaya9: 6-7; Mika 4:3).
Mwisho wa Ufalme wa Milenia ni baada ya miaka 1000 ya utawala wa Kristo hapa duniani. Baada ya miaka hiyo ufalme wa milemnia utachukua sura mpya ya “Ufalme wa Mungu”. Huu utadhihirika kwa matukio makuu matatu:
a) Shetani atafunguliwa baada ya ile
miaka 1000 ya kifungo chake (maana kipindi cha Millenia
hatafurukuta) (Ufunio 20:1-3).
Wakati huo atajipanga kufanya vita (a final show down) dhidi ya Bwana
Yesu Kristo na watakatifu (wateule) lakini atashindwa kabisa katika vita hiyo
kuu sana. Yapo mataifa ambayo yatashikamana na Ibilisi kupigana na Kristokatika
kipindi hichi cha mwisho baada ya milenia lakini watashindwa – Ufunuo 20:7-10 inabainisha haya.
b) Shetani (Ibilisi) atakomeshwa
kabisa na ufalme wake utaondolewa na kukoma kabisa!
c) Waovu wote watahukumiwa na kutiwa
hatiani kwa yale yote yaliyotendwa katika mwili. Hii ni hukumu ya mwisho
(tz.Ufunuo 20:11-15). Haya yote
yatatokea wakati wa mwisho baada ya kipindi cha milenia kumalizika. Watu wote
ambao hawataonekana katika “Kitabu Cha Uzima Cha Mwana-kondoo”
watatupwa katika ziwa la moto, nah ii inaitwa “mauti ya Pili” maana watatengwa na Mungu aliye hai milele na milele!
Ni muhumu basi, ndugu
msomaji wangu mpendwa, kuzingatia sana habari za wokovu huu tuliopewa. Maandika
yanasema sis je tutapata je kupona
tusiojali wokovu huu? Kumbuka kuwa pazia la wokovu lilianza pale Eden na
kudhihirika pale Golgotha! Baadae litakunjwa au
kufungwa baadaye – yaani Mungu ataufunga ukurasi wa maisha ya dunia hii.
Je umesha fanya maauzi ya wapi utakuwa umeangukia? Je ni katika ziwa la moto au
ni katika Paradiso ya Kristo? Katika hayo mawili unapaswa kuyafanyia maamuzi.
Uamuzi wa kumchagua Yesu na kuingizwa katika kitabu cha Uzima cha Mwanakondoo
ni wa maana zaidi kuliko kuishi bila uhakika wa maisha ya sasa na yale ya
baadae.
Mungu akubarikie kwa
kusoma na kuchukua hatua. Kwa maswali zaidi, niandikie: nangela04@yahoo.co.uk
au fuatilia katika blogu hii.
No comments:
Post a Comment