UFALME WA MUNGU: SIFA ZA UFALME WA MILENIA
Utangulizi
Moja ya mambo ambayo Biblia
imeyasisitiza sana ni juu ya ujio wa Ufalme wa Mungu. Ufalme wa Mungu ni
utawala wa Mungu kati ya/juu ya Wanadamu na uumbaji wa Mungu. Katika dhana ya Ufalme wa Mungu ipo dhana
ndogo ya Utawala wa Kristo wa Milenia.
Huu ni ule utawala wa Bwana Yesu katika dunia hii kwa kipindi cha miaka elfu
moja (1000) yaani milenia moja. Katika kipindi hiki:
i.
Kristo Yesu atatawala
ulimwengu wote.
ii.
Israel wote watarejeshwa
pale mashariki ya kati kikamilifu- yaani katika nchi yao ya ahadi (Palestine). Twajua ya kini kwamba Mungu alishaanza haya
tangu mwaka 1948 mara tu baada ya Israel kupata uhuru wake. Hata sasa Mungu yu
kazini kuhusu kutimiza haya ambayo Neno lake lilisha yaweka wazi.
Maandiko
Tuanze
na Nabii Isaya 11:10-12. Hapa Bwana nasema
atawatwekea mataifa bendera na wana wa –Israeli waliotawanyika watakusanywa
toka pande zote nne za ncha za dunia. Kama tulivyobainisha hapo juu, Bwana
alishaanza.
Yeremia
naye hakuacha kusema juu ya jambo hili. (Yer.16:14-15).
Mara ya kwanza Bwana aliwatoa Misri. Mara hii anawatoa katika utawanyiko pande
zote za dunia.
Yer. 30:10 anasema Yakobo atarudi na kutulia.Maana Bwana ndiye
aliyewapanda, nani atawang’oa?
Nabii
Ezekieli naye analo la kusema. Ezek.36:24,
na Ezekie 37 inasema wazi kuwa pamoja na kuwa Israel ilionekana kama bonde
la mifupa, bado Bwana alitangaza maona haya kwa Ezekiel kwamba atawafanya kuwa
Taifa kubwa na lenye nguvu.
Kipindi
tuishicho
Yer. 31:
31-34- inaonyesha matengenezo mapya kwa wana wa Israel. Tena watatubu kama
taifa na kumkubali Kristo kama Bwana wao! Ezekiel
36:24-29 pia inashuhudia juu ya kuwepo urejesho wa wana wa Israel na
kufanywa kwao upya. Mambo haya
yametabiriwa pia katika Zekaria 12:10-11.
Maana nyumba ya Israel itamwona Yesu nao watamwombolezea kama taifa zima. Hivyo
liko taraja kwa taifa la Israel kihusiana na kumwamini Yesu . Kipindi hicho neema ya wokovu
itawageukia zaidi wana wa Israel. Watu wengineo (wa mataifa) wataokoka LAKINI kwa dhiki nyingi! (Rom.11:25-32) Zamu hii ni zamu ya watu wa Mataifa. Neema ya wokovu
imefunuliwa (Tito 2:11-13) Atakaye ipokea atasalimika. Atakaye ikataa
ataangamia maana hukumu na gadhabu ya Mungu itamkalia (Yoh.3:36).
Baada ya utangulizi huu, sehemu inayofuata
ataangazia juu ya Utawala wa Kristo katika Millenia utakavyokuwa.
·
Utakuwepo wakati wa
AMANI kuu na baraka pote ulimwenguni katika kipindi cha utawala wa Yesu wa
Milenia.
·
Dunia itageuzwa na
kubadilishwa maana viumbe vya asili vitafunguliwa katika kifungo kilichotokana
na dhambi. Ukisoma Warumi 8:19-22, inasema viumbe vinayoshauku (matarajio
makuu) ya kufunuliwa kwa Yesu Kristo.
Kwa sasa vinaumia kwa sababu ya dhambi. Maana navyo vitawekwa huru katika
utumwa na uharibifu.
·
Isaya 35:1-2 inaonesha
jinsi ambavyo katika kipindi hicho Bwana atafanya mambo mengi kuwa mapya.
Ezekieli 34:26-27 nayo inathibitisha pia. Maradhi yataondolewa na miaka ya
wanadamu itaongezeka. Isaya 35:5-6; na Isaya 65:20-25 inaonesha hilo! Hata mtu
wa miaka 100 moja ataonekana kuwa motto. Maandiko yanasema kama zilivyo siku za
mti ndivyo zitakavyokuwa siku za watu wa Mungu katika kipindi cha milenia ya
Kristo!
(….itaendelea sehemu ya pili….)
Ni muhimu kutambua
mambo haya kwani Kanisa ni wakala wa Ufalme wa Mungu. Wokovu wetu uliandaliwa
na Bwana mwenyewe.Ufalme wa Mungu ni wa milele na si wa kitambo kama zilivyo
famlme za kidunia! Kanisa , kama wakala wa Ufalme wa mungu, lipo kwa kipindi tu
hata ajapo Mfalme mwenyewe, yaani Kristo naye atatawala pamoja na watakatifu.
Swali kubwa ni je? Umejiweka tayari? Kama wewe umesoma sehemu hii na ukajiona
kuwa umepungukiwa mbele za Mungu, bado iko nafasi kwani mlamgo wa neema uko
wazi . Unaweza kutengeneza maisha yako na Mungu kwa kutubu na kumwamini Yesu!
Unaweza kuokolewa tu kwa toba na Imani katika Kristo Yesu. Ukimpata Yesu
umeupata ufalme maana mwenye ufalme ni Mfame mwenyewe! Leo fanya maamuzi. KUOKOKA NI UAMUZI WAKO!